Tunavyo Tegemeana Kwenye Mazingira

Date:

Share post:

Tunavyo Tegemeana Kwenye Mazingira

Lazimu tukubaliane na ukweli kwamba kila alichokiumba Mungu kipo kwa sababu maalumu, na kina faida  kwa uwepo wake hapo kilipo. Hakuna ambacho hakina maana kwa viumbe hai wote walioumbwa na Mungu kila kitu kina maana yake ya kuwepo. Changamoto yetu kubwa ni kutokujua sababu ya uwepo wa kitu hicho, hivyo hupelekea matumizi na maamuzi yasiyosahihi kwa mtumiaji.

Uwepo wa maliasili zetu zenye thamani kubwa ni jambo ambalo kama nchi tunajisifia na kumshukuru Mungu kwa kuruhusu wanyama hawa na maliasili hizi kuendelea kukaaa hapa. Tunazungukwa na mandhari nzuri sana iliyopambwa na hali nzuri ya hewa na ya utulivu iliyochangiwa na uwepo wa misitu na mapori mengi sana yenye kuvutia na kuifanya nchi yetu kutokuwa kati ya nchi zisizoathiriwa na hali ya jangwa .

Kwa asilimia kubwa vitu hivi vinachangia kwa kiasi kikubwa muendelezo wa maisha ya binadamu hapa duniani. Kwa mfano mwadamu ili aweze kuishi anahitaji hewa ya Oksijeni ambayo hutolewa na uwepo wa miti ya kutosha kwenye maeneo yetu. Na ili mimea iendelee kukua na kujitengenezea chakula chake unahitaji hewa ya kabonidayoksaid ambayo hutolewa na binadamu na kutumiwa na mimea. Hivyo kuendelea kuwepo kwa wanyama wanaokula nyasi na majani unategemea binadamu. Vilevile jinsi ambavyo majani yanakuwa mengi na yakutosha yanavutia kwa kiasi kikubwa wanyama kama wa aina mbali mbali, wanaokula majani na wanao kula nyama.

Tunapotunza wanyama hatutunzi tu wanyamapori bali tunatunza na hata mazingira yanayosababisha uwepo wa wanyama hawa. Hivyo inakuwa tunaweza kutengeneza uwiano mzuri kati yetu na wanyama hawa. Tunataka serikali, wadau na wanajamii ya kuwa mradi huu ni muhuimu ni jukumu letu muhimu sana.

Sisi kama wadau wa mazingira na maliasili zote Tanzania tunatakiwa kujifunza tabia za hawa watu kwa  kuishi nao karibu. Tuwaonyeshe namna ya kukaa na kuchukuliana na wenyema .

Makala hii imeandikwa na

Hillary Mrosso

0742092569

hillarymrosso@rockmail.com

 

 

Leave a reply

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

Mimea Dawa na Misitu Ilivyo Muhimu kwa Maisha ya Sasa na Baadaye

Siku ya wanyamapori duniani inatukumbusha kutafakari namna tunavyoishi na mazingira yanayotuzunguka. Mazingira kama misitu, miti, maji, hali ya...

Safari ya Hillary Thomas Mrosso Katika Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania

Wakati nasoma elimu ya msingi na sekondari, nilikuwa na ndoto za kuwa daktari wa binadamu, hivyo nilipenda sana...

Zijue Sababu za TAWIRI Kukataa Matokeo ya Utafiti wa Duporge na Wenzake Kuhusu Idadi ya Nyumbu Katika Eneo la Serengeti – Masai Mara,...

Uhifadhi endelevu wa wanyamapori unahitaji tafiti za kina za mara kwa mara kwa kutumia mbinu sahihi zilizohakikiwa ili...

SHAIRI: Tutunze Makazi ya Simba

1.Ndugu zangu karibuni, nina jambo kutamka Simba wapo hatarini, majangili wawasaka Waharibu masikani, kuvuka yao mipaka Simba wanayo thamani, tutunze makazi...