SHAIRI: Tutunze Makazi ya Simba

Date:

Share post:

Picha imepigwa na Hillary Mrosso, katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere, Tanzania

1.Ndugu zangu karibuni, nina jambo kutamka
Simba wapo hatarini, majangili wawasaka
Waharibu masikani, kuvuka yao mipaka
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

2.Simba waisha porini, hali sipobadilika
Hatua tuchukueni, tusije tukaumbuka
Wabaya tuwajueni, ikibidi kuwashika
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

3.Mikakati tuwekeni, ujangili tumechoka
Mizaha tweke pembeni, na tuingiwe mashaka
Sijekuwa masikini, uchumi wetu kushuka
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

4.Zaja hela za kigeni, Utalii kifanyika
Tutafuta na madeni, nchi itaheshimika
Tutatamba duniani, washindi tutaibuka
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

5.Simba haba hifadhini, malaki hawajafika
Waweza usiamini, lakini waongezeka
Siweke silaha chini, bado hatujaridhika
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

6.Kalamu naweka chini, nimechoka kuishika
Nimefikia mwishoni, wa shairi kuandika
Wekeni haya moyoni, daima kuyakumbuka
Simba wanayo thamani, tutunze makazi yao

Hillary Mrosso| mrossotm@gmail.com
+255 683 862 481 |Morogoro| 10.08.2025

Leave a reply

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

Mimea Dawa na Misitu Ilivyo Muhimu kwa Maisha ya Sasa na Baadaye

Siku ya wanyamapori duniani inatukumbusha kutafakari namna tunavyoishi na mazingira yanayotuzunguka. Mazingira kama misitu, miti, maji, hali ya...

Safari ya Hillary Thomas Mrosso Katika Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania

Wakati nasoma elimu ya msingi na sekondari, nilikuwa na ndoto za kuwa daktari wa binadamu, hivyo nilipenda sana...

Zijue Sababu za TAWIRI Kukataa Matokeo ya Utafiti wa Duporge na Wenzake Kuhusu Idadi ya Nyumbu Katika Eneo la Serengeti – Masai Mara,...

Uhifadhi endelevu wa wanyamapori unahitaji tafiti za kina za mara kwa mara kwa kutumia mbinu sahihi zilizohakikiwa ili...

Shairi: Agosti kumi ya Simba

Leo twendeni mbugani, utalii mbuga zetu Huko leo kuna nini, nataka ninene kitu Leo huko duniani, siku ya bingwa wa...