More

    Wafahamu Wanyama Na Ndege Wote Waliotajwa Kwenye Jedwali La Kwanza La Sheria Ya Wanyamapori

    Habari msomaji wa makala za wildlife Tanzania, karibu kwenye makala ya leo ambayo tunaendelea kuichambua  Sheria ya wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009. Tukiwa tunaelekea mwishoni mwa uchambuzi wa sheria hii, nataka ujue wanyama na ndege waliotajwa sana kwenye baadha ya sehemu za sheria hii. Wakati tunaanza uchambuzi wa sheria hii kuna vifungu vingi sana vinataja wanyama ambao wapo kwenye majedwali ya sheria hii. Sasa leo tutaona jedwali la kwanza na wanyama waliopo kwenye sehemu hii ya jedwali. Kwenye sheria ya wanyamapori wametumia majina matatu kwa lugha ya Kiswahili, kingereza na jina la kisayansi wakati wa kuwataja wanyama na ndege hawa.

    Jina la kiswahili Jina la kingereza Jina la Kisayansi
    Babakoko sanje Sanje Mangabay Cercocebus sanjei
    Choroa Oryx Oryx beisa callotis
    Chui Leopard Panthera Padus
    Duma Cheetah Acinonyx jubatus
    Faru Black Rhinoceros Diceros bicornis
    Kipunji Highland Mangabey Lophocebus kipunji
    Mbuzi mawe (Nguru) Klipsgringer Oreotragus oreotragus
    Mbwa mwitu Wild dog Lycon pictus
    Mindi Abbotts Duiker Cephalophus Spadix
    Nyati (Mbogo) Buffalo Snycerus caffer caffer
    Nzohe Sitatunga Limnotragagus spekeii
    Pahalahala rosaveti Rosavelt Sable Hipotragus niger rosalvetii
    Pimbi Hyrax Heterohyrax/Procavia
    Pundamilia Zebra Equus burchellii
    Sengi Giant Elephant Shrew Rynochocyon uduzungwensis
    Sheshe Puku Kubus vardoni
    Simba Lion Panthera leo
    Simbamangu Caracal Felis caracal
    Swala robati Robart Gazzele Gazella granti robartsi
    Swalatwiga Gerenuk Litocranus walleri
    Tandala mdaogo Lesser Kudu Strepsiceros imberbis
    Tembo (Ndovu) African Elephant Loxodonta Africana
    Tohe- mlima Mountain Reedbuck Redunca fulvorufula
    Korongo nyangumi Shoebill (Whale headed stock) Balaeniceps rex
    Korongo usomwekundu Watle Crane Bugeranus carunculatus
    Kozi kipanga Peregrin Falcon Falco peregrinus
    Kwale uduzungwa Uduzungwa Forest Patridge Xenoperdix uduzungwaensis
    Ninga Green Pigion Treron
    Mamba Slender Snorted Crocodile Crocodilus crataphractus
    Chura wa Kihansi Kihansi Spray Toad Nectophrynoides asperginis

    Hivyo Rafiki naamini kabisa utakaposoma makala au seheria wakitaja wanyama waliopo kwenye majedwali basi nadhani utaelewa vizuri kabisa. Leo nimetaja tu wale wanyama na ndege wanaopatikana kwenye Sehemu ya kwanza ya Jedwali na jedwali la kwanza. Karibu kwa maswali na maoni, bila kusahau ushauri.

    Ahsante sana!

    Hillary Mrosso

    Wildlife Conservationist

    +255 683 248 681/+255 742 092 569

    hillarymrosso@rocketmail.com

    www.mtaalamu.net/wildlifetanzania

    Latest articles

    Related articles

    Leave a reply

    Please enter your comment!
    Please enter your name here