Barua Ya Wazi 8; Nawawatakia Kheri Ya Krismasi Wahifadhi Na Wasomaji Wetu Wa Masuala Ya Maliasili

Date:

Share post:

Habari msomaji wa makala za wildlife Tanzania, karibu kwenye makala ya leo, ni makala ambayo nimepanga kukushukuru na kukutakia kila la kheri kwenye mapumziko haya ya sikukuu za Krismasi. Najua katika kipindi kama hiki watu wengi wapo majumbani kwao na familia zao, wengine bado wanaendelea kupambana na shughuli za kila siku. Lakini yote katika yote nawatakia mapumziko mema na mazuri katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu.

Kuna wengine wamepanga kutembelea maeneo ya vivutio na mbuga za wanyama kwenye msimu huu wa sikukuu, kuna wengine wapo nyumbani na familia zao, yote ni mema. Nami nawapongeza na kuwaakia kila la kheri. Makala ya leo haitakuwa na mambo mengi sana, ni makala ya kuwatakia kila la kheri kila msomaji wetu na kila mtanzania.

Naamini umekuwa ukisoma makala zetu kwenye blog ya wildlife Tanzania, ambapo tunaandika makala mpya kila siku na kuzichapisha huko, makala hizi ni kwa ajili ya kuhamasisha utalii na uhifadhi wa wanyamapori, pia makala hizi ni kwa ajili ya utunzaji wa mazingira, hivyo kwa kiasi chake naamini umepata maarifa na taarifa muhimu, na kujifunza mambo mbali mbali ya wanyamapori.

Pia nataka kukufahamisha kuwa uandishi wa maswala haya ya wanyamapori ni jambo ambalo napenda kulifanya na pia napenda kuandika habari nyingi zenye kuleta hamasa na maarifa kwa watanzania na kwa kila mtu kuhusu uhifadhi na utalii wa ndani. Naamini katika njia hii itasaidia na kutoa mwanga kwa watanzania wenzetu wasio na uelewa wa mambo haya, lakini pia kupitia makala hizi watu watawajua wanyama, watawapenda na watakuwa tayari kuwatunza na kuwahifadhi.

Nakushukuru kwa kuendelea kufuatilia na kuwa msomaji wa makala za mtandao wetu wa www.mtalaam.net/wildlifetanzania . Nakuahidi mambo mazuri yanakuja mambo ya kuelimisha na kufahamu zaidi hifadhi zetu na vivutio mbali mbali. Karibu tuendele kuwa pamoja kujifunza, kufurahia na kutembelea, mambo mengi mazuri yanakuja.

Asante sana kwa kusoma makala hii, karibu kwa makala nyingine.

Hillary Mrosso

Wildlife Conservationist

+255 683 862 481/+255 742 092 569

hillarymrosso@rocketmail.com

www.mtaalamu.net/wildlifetanzania

Leave a reply

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

Mimea Dawa na Misitu Ilivyo Muhimu kwa Maisha ya Sasa na Baadaye

Siku ya wanyamapori duniani inatukumbusha kutafakari namna tunavyoishi na mazingira yanayotuzunguka. Mazingira kama misitu, miti, maji, hali ya...

Safari ya Hillary Thomas Mrosso Katika Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania

Wakati nasoma elimu ya msingi na sekondari, nilikuwa na ndoto za kuwa daktari wa binadamu, hivyo nilipenda sana...

Zijue Sababu za TAWIRI Kukataa Matokeo ya Utafiti wa Duporge na Wenzake Kuhusu Idadi ya Nyumbu Katika Eneo la Serengeti – Masai Mara,...

Uhifadhi endelevu wa wanyamapori unahitaji tafiti za kina za mara kwa mara kwa kutumia mbinu sahihi zilizohakikiwa ili...

SHAIRI: Tutunze Makazi ya Simba

1.Ndugu zangu karibuni, nina jambo kutamka Simba wapo hatarini, majangili wawasaka Waharibu masikani, kuvuka yao mipaka Simba wanayo thamani, tutunze makazi...