Kwa Wasomaji Wa Blog Ya Wildlife Tanzania

Date:

Share post:

Habari mtanzania mwenzangu, hongera kwa siku ya leo. Leo ni siku ya kipekee ambayo tunakwenda kuangalia baadhi ya mambo muhimu kwenye utalii wetu na kwenye maliasili zetu. Hivyo karibu tuone mambo mbali  mbali na vivutio mbali mbali vilivyopo hapa duniani. Ni baadhi ya maneno ambayo nimekuwa nikayatumia sana kwenye uandishi wa makala za wildlife Tanzania, hivyo nimeyaelezea maneno haya kwa ufupi ili upate picha kubwa ninayotaka uione kwenye makala na maliasili zetu za Tanzania. Hivyo karibu fuatana nami kwenye makala hii.

Mtalii

  • Ni mtu anaye safari na kwenda nje ya mahali alipokuwa mwanzo
  • Ni mtu anayesafiri kwenda kwenda kwenye mazingira tofauti na aliyozoea
  • Ni kwenda maeneo kutembelea maeneo ya vivutio kwa muda usiozidi mwaka mmoja
  • Ni mtu anayesafiri kwenda mbali na mazingira ya nyumbani kwa sababu mbali mbali, kama vile starehe, biashara, au sababu nyingine.

Vivutio

  • Ni kitu kinachofurahisha na kusisimua
  • Ni kitu kinachoteka na kukufanya ushangae
  • Ni sehemu inayovutia na kushawishi watu kwenda kutembelea
  • Ni vitu au kitu ambacho ni kigeni ambacho kila mtu anavutika kukiangalia
  • Ni vitu ambavyo huwafanya watu wasafiri kuona vitu hivyo

Vivutio vya Kitalii

  • Ni vitu ambavyo vinavyofanya watu wasafiri kuona vitu hivyo
  • Ni sehemu yenye maajabu ambayo kila mtu anatamani kuviona
  • Vitu hivi vinaweza kuwa;
  • Utamaduni
  • Hali ya hewa
  • Asili
  • Uoto wa asili
  • Makumbusho
  • Sehemu za kihistoria
  • Sehemu zenye miji mikubwa
  • Maporomoko ya maji
  • Majangwani
  • Misitu minene
  • Mbuga za wanyama
  • Wanyamapori waliofugwa (zoos)
  • Bahari
  • Mito
  • Mabwawa ya maji
  • Maeneo oevu
  • Maeneo yenye viwanda na mitambo mikubwa
  • Milima na miinuko
  • Tambarare zenye nyasi na mchanga
  • Fukwe za bahari
  • Kwenye maonyesho mbali mbali
  • Kwenye visiwa mbali mbali
  • Sehemu zenye mashamba makubwa
  • Sehemu zenye mawe na miamba
  • Sehemu zenye miti mikubwa yenye mapango
  • Sehemu zenye ndege wengi
  • Maeneo yenye mahoteli makubwa
  • Maeneo yenye biashara sana

Kuna maeneo mengi sana ya kutembelea kwa hapa Tanzania na duniani kwa ujumla, hivyo elewa nini kinakuvutia zaidi na jipange kwenda kutembelea, nenda katembelee, nenda tu sio tu kwamba utaburudika na kufurahia bali utajifunza sana mbinu mbali mbali za maisha na maisha yako yatakuwa bora.

Kuna maeneo mengi sana hapa nchini yametengwa kwa ajili ya viumbe hai na maliasili nyingine muhimu sana. Mengine yanalindwa na sharia kali sana kwa sababu ya umuhimu wake kwenye ikologia ya viumbe hai. Hivyo nimeainisha baadhi ya maeneo ambayo yanawafanya watu wengi kuvutika na kupanga safari kutembelea maeneo hayo.

Hillary Mrosso

Wildlife conservationist

0742092569/0683248681

hillarymrosso@rocketmail.com

htt://www.mtalaamu.net/wildlifetanzania

 

 

1 Comment

Leave a reply

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

Mimea Dawa na Misitu Ilivyo Muhimu kwa Maisha ya Sasa na Baadaye

Siku ya wanyamapori duniani inatukumbusha kutafakari namna tunavyoishi na mazingira yanayotuzunguka. Mazingira kama misitu, miti, maji, hali ya...

Safari ya Hillary Thomas Mrosso Katika Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania

Wakati nasoma elimu ya msingi na sekondari, nilikuwa na ndoto za kuwa daktari wa binadamu, hivyo nilipenda sana...

Zijue Sababu za TAWIRI Kukataa Matokeo ya Utafiti wa Duporge na Wenzake Kuhusu Idadi ya Nyumbu Katika Eneo la Serengeti – Masai Mara,...

Uhifadhi endelevu wa wanyamapori unahitaji tafiti za kina za mara kwa mara kwa kutumia mbinu sahihi zilizohakikiwa ili...

SHAIRI: Tutunze Makazi ya Simba

1.Ndugu zangu karibuni, nina jambo kutamka Simba wapo hatarini, majangili wawasaka Waharibu masikani, kuvuka yao mipaka Simba wanayo thamani, tutunze makazi...