More

    Orodha Ya Ndege Wa Kuwindwa (Game Birds)

    Habari msomaji wa makala za wildlife Tanzania, karibu kwenye makala nyingine ya leo, ni makala nzuri sana, kwa sababu itakujuza mambo mengi ambayo huyajui kuhusu wanyama na ndege, kwa mujibu wa sheria ya wanyamapori ya mwaka 2009.  Sehemu ya mwisho kabisa mwa sheria hii kuna majedwali yanayotaja wanyama na ndege wengi ambao wengine hatuyajui majina yake. Jana tulijifunza big game wote ambao wapo kwenye sheria hii sehemu ya tatu na jedwali la tatu. Leo tuendelee na jedwali la tatu (Third Schedule). Jana tulijifunza wanyama, lakini kwenye makala ya leo tutajifunza kuhusu ndege. Karibu sana tujifunze pamoja tuwaangalie Game birds wote waliopo kwenye sheria hii, ( ninaposema game birds maana yake ndege wanaoruhusiwa kuwindwa au wakuwindwa, lakini wanawindwa kwa kibali maalumu kabisa.

    Katika majina haya yametajwa jina la Kiswahili, kingereza, na jina la kisayansi.

    Jina la Kiswahili Jina la Kingereza Jina la Kisayansi
    Bata bukini mdogo Piggmy Goose Nettapus
    Bata bukini Egyptian Goose Alopochen
    Bata bukini- bawa kijani Spurwing Goose Plectropterus
    Bata domo – kifundo Knob-billed Goose Sarkidiornis
    Bata kichwa chekundu Northern Pochard Aythya
    Bata kichwa cheupe White Faced Whislting Ducks Dendrocyna
    Bata mdogo Teals Anas
    Bata- makoa Maccoa Duck Oxyura
    Firiogo koo-njano Yellow- Throated Sandgrouse Pterocles
    Firingogo tumbo jekundu Chestnut- bellied Sandgrouse Pterocles
    Kanga Helmeted Guinea Fowl Numida
    Keren’gende Pur Fowl Francollinus
    Kituitui tambo Harlequail Quail Cortunix
    Kituitui Common Quail Cortunix
    Kololo Crested Guinea Fowl Guttera
    Kololo tumbusi Vulturine Guinea Fowl Acryllium
    Kotwa White- Backed Duck Thalasomis
    Kwale Francolins Francollinus
    Ninga Green Pigeon Treron
    Njiwa Pigeons Columba
    Pungi Doves Oena
    Pungi Doves Turtur
    Tetere Doves Streptopelia

     

    Hivyo kufikia hapa nikuache na makala hii, ujifunze na kujua ndege waliotajwa kwenye sheria ya wanyamapori, wapo  aina na spishi nyingi sana za ndege. Hawa ndege niliowataja hapa ni kwa mujibu wa sheria mama ya wanyamapori ya mwaka 2009.  Hivyo nikukaribishe kuendelea kujifunza kupitia makala hizi za wanyamapori.

    Ahsante sana!

    Hillary Mrosso

    Wildlife Conservationist

    +255 683 248 681/+255 742 092 569

    hillarymrosso@rocketmail.com

    www.mtaalamu.net/wildlifetanzania

     

    Latest articles

    Related articles

    Leave a reply

    Please enter your comment!
    Please enter your name here