Habari msomaji wa makala za wildlife Tanzania, karibu kwenye makala nyingine ya leo, ni makala nzuri sana, kwa sababu itakujuza mambo mengi ambayo huyajui kuhusu wanyama na ndege, kwa mujibu wa sheria ya wanyamapori ya mwaka 2009.  Sehemu ya mwisho kabisa mwa sheria hii kuna majedwali yanayotaja wanyama na ndege wengi ambao wengine hatuyajui majina yake. Jana tulijifunza big game wote ambao wapo kwenye sheria hii sehemu ya tatu na jedwali la tatu. Leo tuendelee na jedwali la tatu (Third Schedule). Jana tulijifunza wanyama, lakini kwenye makala ya leo tutajifunza kuhusu ndege. Karibu sana tujifunze pamoja tuwaangalie Game birds wote waliopo kwenye sheria hii, ( ninaposema game birds maana yake ndege wanaoruhusiwa kuwindwa au wakuwindwa, lakini wanawindwa kwa kibali maalumu kabisa.

Katika majina haya yametajwa jina la Kiswahili, kingereza, na jina la kisayansi.

Jina la Kiswahili Jina la Kingereza Jina la Kisayansi
Bata bukini mdogo Piggmy Goose Nettapus
Bata bukini Egyptian Goose Alopochen
Bata bukini- bawa kijani Spurwing Goose Plectropterus
Bata domo – kifundo Knob-billed Goose Sarkidiornis
Bata kichwa chekundu Northern Pochard Aythya
Bata kichwa cheupe White Faced Whislting Ducks Dendrocyna
Bata mdogo Teals Anas
Bata- makoa Maccoa Duck Oxyura
Firiogo koo-njano Yellow- Throated Sandgrouse Pterocles
Firingogo tumbo jekundu Chestnut- bellied Sandgrouse Pterocles
Kanga Helmeted Guinea Fowl Numida
Keren’gende Pur Fowl Francollinus
Kituitui tambo Harlequail Quail Cortunix
Kituitui Common Quail Cortunix
Kololo Crested Guinea Fowl Guttera
Kololo tumbusi Vulturine Guinea Fowl Acryllium
Kotwa White- Backed Duck Thalasomis
Kwale Francolins Francollinus
Ninga Green Pigeon Treron
Njiwa Pigeons Columba
Pungi Doves Oena
Pungi Doves Turtur
Tetere Doves Streptopelia

 

Hivyo kufikia hapa nikuache na makala hii, ujifunze na kujua ndege waliotajwa kwenye sheria ya wanyamapori, wapo  aina na spishi nyingi sana za ndege. Hawa ndege niliowataja hapa ni kwa mujibu wa sheria mama ya wanyamapori ya mwaka 2009.  Hivyo nikukaribishe kuendelea kujifunza kupitia makala hizi za wanyamapori.

Ahsante sana!

Hillary Mrosso

Wildlife Conservationist

+255 683 248 681/+255 742 092 569

hillarymrosso@rocketmail.com

www.mtaalamu.net/wildlifetanzania