Shairi: Agosti kumi ya Simba

Date:

Share post:

Picha imepigwa na Sheridan Wright, katika hifadhi ya taifa ya Serengeti, Tanzania

Leo twendeni mbugani, utalii mbuga zetu
Huko leo kuna nini, nataka ninene kitu
Leo huko duniani, siku ya bingwa wa mwitu
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwatunze

Simba ni bingwa wa mwitu, hakuna asiyejua
Anaogopwa na watu, na mbio wakatimua
Mnyama ni mthubutu, mwendo wake wa hatua
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwalinde

Simba huyu maarufu, kivutio duniani
Ila twaingia hofu, wachache wasothamini
Ni watu waharibifu, wawawindao porini
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwatunze

Tudhibiti majangili, waletao maumivu
Tuwe na moja kauli, na pamoja zetu nguvu
Mbinu zote mbalimbali, dhidi ya wa nia ovu
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwalinde

Tusifunge yetu macho, kila mara tuwalinde
Hadi kizazi kijacho, watusifu watupende
Kuwa tulikuwa jicho, wasituponde ponde
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwatunze

Siku hii ya Simba, tulinde hii zawadi
Hata simba mwenye mimba, alindwe tena zaidi
Kutolinda ni kuchimba, shimo letu makusudi
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwatunze

Kuwatunza ni muhimu, kivutio cha wageni
Tuwalinde zamu zamu, pato lisishuke chini
Wakiwa hawa adimu, tutapotea sokoni
Agosti kumi ya Simba, ni jukumu tuwalinde

Malenga wa Ubena
+255 676 559 211
Uhifadhi
Wildlife Tanzania

1 Comment

Leave a reply

Please enter your comment!
Please enter your name here

spot_img

Related articles

Mimea Dawa na Misitu Ilivyo Muhimu kwa Maisha ya Sasa na Baadaye

Siku ya wanyamapori duniani inatukumbusha kutafakari namna tunavyoishi na mazingira yanayotuzunguka. Mazingira kama misitu, miti, maji, hali ya...

Safari ya Hillary Thomas Mrosso Katika Uhifadhi wa Wanyamapori Tanzania

Wakati nasoma elimu ya msingi na sekondari, nilikuwa na ndoto za kuwa daktari wa binadamu, hivyo nilipenda sana...

Zijue Sababu za TAWIRI Kukataa Matokeo ya Utafiti wa Duporge na Wenzake Kuhusu Idadi ya Nyumbu Katika Eneo la Serengeti – Masai Mara,...

Uhifadhi endelevu wa wanyamapori unahitaji tafiti za kina za mara kwa mara kwa kutumia mbinu sahihi zilizohakikiwa ili...

SHAIRI: Tutunze Makazi ya Simba

1.Ndugu zangu karibuni, nina jambo kutamka Simba wapo hatarini, majangili wawasaka Waharibu masikani, kuvuka yao mipaka Simba wanayo thamani, tutunze makazi...