Biashara ya wanyamapori na mimea mwitu ni muhimu hapa duniani kwa ajili ya kukidhi baadhi ya mahitaji muhimu ya binadamu, tunahitaji wanyamapori na mimea kwa sababu mbali mbali kama vile chakula, dawa, nguo na hata kwa matumizi ya ujenzi wa nyumba au sehemu za kuishi. Hivyo kwa namna yoyote ile uwepo wa wanyamapori ni muhimu sana kwa ajili ya kukidhi baadhi ya mahitaji hayo muhimu.

Kwasababu hiyo, tumekuwa tunatumia rasilimali hizi ambazo kwa kiasi kikubwa zipo kwenye maeneo yetu na nyingine zimehifadhiwa na kusimamiwa na sheria kali ili kuepuka matumizi ambayo sio endelevu. Msingi wa uhifadhi wa wanyamapori na mimea mwitu, au misitu ni kwa ajili ya kutumiwa kwa uendelevu ili kuhakikisha rasilimali hizi zinaendelea kuwepo kwa faida ya vizazi vingi vya sasa na badaye.

Moja ya spishi za Hondo hondo zinazopatikana kwa wingi katika nchi ya Indonesia sasa zimeingia katika orodha ya spishi ya ndege walio hatarini kutoweka, hii ni kwa mujibu wa makala iliyoandikwa na Serene C.L katika jarida la Traffic bulletin iliyotoka Oktoba 2017, mwandishi ana ainisha namna ambavyo idadi ya ndege hawa ilivyokuwa kubwa, lakini sana idadi yao imeshuka kutokana na uhitaji wake kwenye nchi mbali mbali za Asia.

Kutokana na ujangili uliokithiri wa ndege hawa, mwaka 2015 ndege hawa waliingia katika orodha ya ndege ambao wamo hatarini kutoweka. Taarifa za kina zinaonyesha zaidi ya matukio tofauti tofaut 59 ya ukamataji wa nyara za ndege hawa, ambapo zaidi ya nyara 2878 za sehemu mbali mbali za ndege hawa zilikamatwa, ikiwa ni pamoja na kichwa ambacho ndio nyara kuu inayohitajika na watumiaji wa ndege hawa.

Kama ilivyo kwa ujangili wa wanyamapori wengine kama vile tembo na faru, majangili wa ndege hawa wana mtandao mkubwa sana unaohusisha watu mbali mbali ambao husaidia katika uasafirishaji wa nayara hizo kutoka Indonesia hadi China ambako ndio watumiaji wakuu wa nyara hizo za horn bill au hondo hondo.

Ili kukabiliana na tatizo hilo, ilifanyika washa iliyojulikana kama Helmented Hornbill Conservation and Actio Planning ambayo ilifanyika Sarawk Malasia kuanzia tarehe 19 – 20 Mai 2017. Ambapo watalamu 36, watekelezaji, mamlaka za wafanya maamuzi ambao walikuwa serikali kutoka China, Indonesia, Thailand na Malasia, pia walikuwepo watafiti na mashirika mmbali mbali yasiyo ya kiserikali. Lengo kuu la kuita wakuu wote na watalamu mbali mbali ilikuwa ni moja, ni kwa namna gani kwa kushirikiana wote kwa pamoja wanaweza kusaidia ndege hawa wasitoweke hapa duniani. Pamoja na kuafikiana mipango na mikakati ya kuwanusuru ndege hawa, pia walipata kuungwa mkono na mashirika makubwa kama vile IUCN, WCS, nk.

Pia katika warsha hiyo walikubaliana kwa pamoja kuainisha mambo yote yanayotishia kutoweka kwa ndege hawa, baadhi ya mambo waliyokubaliana kufanya kwa pamoja ili kuokoa spishi za ndege hawa ni kujenga ufahamu kujua mtawanyiko, ikoloia na baiolojia ya ndege hawa, jambo la pili walikubaliana kuelewa madhara yanayoletwa na uharibifu wa makazi ya ndege hawa, ukame na uvamizi wa maeneo ya ndege hawa, jambo la tatu walikubaliana kuhusu biashara ya ndege hawa, utekelezaji wa sheria na sera za usimamizi wa nedge hawa na maeneo yake muhimu na jambo la nne na la mwisho walikubaliana kuharibu kabisa biashara na mtandao wote wa majangili na watumiaji wa nyara za ndege hawa.

Pia ili kuhakikisha waliyokubaliana yanaanza kufanyiwa kazi mara moja, kwa pamoja walikubaliana kuunda kikundi kitakachojihusisha kwa ukaribu na ndege hawa, mfano wa kikundi hicho waliamua kukiita helmented Hornbill working group, ambacho kitafanya shughuli zake zote chini ya mwavuli wa shirika la IUCN.

Kazi yao kubwa itakuwa kuhakikisha utekelezaji wa makubaliano ya wajumbe waliyoridhia yanafanyiwa kazi. Pamoja na mambo mengine kikundi hicho kilichoundwa kitakuwa na wajibu wa kushirikiana na taasisi mbali mbali za utafiti wa ndege hawa, kushauri serikali kuhusiana na hali na mwenendo wa spishi hizo za ndege. Kazi yote hiyo ni kuhakikisha kila walichokubaliana kwenye mkutano kuhusiana na uhifadhi wa ndege hawa kinafanyiwa kazi mapema.

Baada ya kusoma makala hii katika jarida la traffic bulletin, nimeona mambo mengi ambayo kwa pamoja kama wahifadhi tunaweza kuyafanyia kazi ili kuendeleza uhifadhi wenye tija. Wepesi wa kutekeleza yale muhimu waliyokubaliana kwenye vikao na mikutano ni jambo jingine muhimu la kujifunza siku zote. Wote tunaofanya kazi katika sekta hii ya maliasili tunahitaji taarifa za aina hii kwa ajili ya kujua na kujiandaa, kwasababu majangili wa spishi za ndege hawa wanaweza kuhamia kwenye hifadhi zetu na kuanza kutusumbua. Tujifunze na tuchukua hatua!

Nakushukuru sana Rafiki kwa kusoma makala hii hadi mwisho, naamini umepata mwanga kwenye masuala haya ya uhifadhi wa maliasili zetu. Karibu tuendelee kujifunza zaidi kwenye makala ijayo hapa hapa kwenye mtandao wako wa Wildlife Tanzania. Pia usiache kuwashirikisha wengingi haya uliyojifunza hapa.

Hillary Mrosso

+255 683 862 481

hillarymrosso@rocketmail.com

www.mtalaam.net/wildlifetanzania